HIVI NDIVYO BRELA INAVYOIWEKA BIASHARA YAKO KATIKA MIKONO SALAMA



USAJILI WA KAMPUNI

Kampuni ni nini?

Kampuni ni mjumuiko wa watu wawili au zaidi wenye nia ya kufanya biashara halali na kuusajili mjumuiko huo chini ya Sheria ya kampuni.

Aina za Kampuni

Kampuni ya kigeni

Kampuni binafsi

Kampuni ya umma

Faida za Urasimishaji Kampuni ni zipi?

Kuipatia utu wa kisheria biashara yako

Kutambulika na taasisi za fedha mf. bienki wakati wa kufungua akaunti.

Kupata mikopo katika taasisi za fedha kama benki.

Kupanua wigo wa kufanya biashara kubwa, mf. biashara za kimataifa

Urahisi wa kuitangaza kampuni kwa urahisi na kupanua wigo wa wateja.

Vigezo vya kusajili Kampuni

Mwombaji anatakiwa kuwa na namba ya kitambulisho cha Taifa kutoka NIDA

Namba ya kitambulisho cha Taifa kutoka NIDA ya kila mwanahisa

Namba ya kitambulisho cha Taifa kutoka NIDA au pasi ya kusafiria kwa raia wa kigeni na namba ya utambulisho wa mlipakodi (TIN) ya kila mkurugenzi

Nyaraka za kuambatisha

Katiba ya Kampuni

Fomu ya uadilifu

Fomu ya majumuisho (Consolidated Form)

Hatua 10 za kusajili Kampuni

Tembelea "www.brela.go.tz" au "ors.brela.go.tz".

Ingia katika akaunti yako ya Usajili kwa njia ya mtandao (ORS) au tengeneza akaunti katika mfumo.

Chagua "huduma mtandao".

Chagua "kampuni".

Chagua "aina ya huduma".

Chagua "aina ya kampuni".

Jaza taarifa za kampuni husika.

Pakia viambatisho katika mfumo.

Lipa kwa njia ya simu au benki.

Maombi yatafanyiwa kazi baada ya malipo kupokewa.

Post a Comment

Previous Post Next Post