DAS Kinondoni aonya wazazi, walezi kuwalinda watoto dhidi ya ukatili



Na Mwandishi Wetu

Wazazi na walezi wanaowapeleka watoto katika shule za bweni wakiwa bado wadogo wameshauriwa kuwafuatilia kwa karibu katika makuzi yao wakiwa shuleni na wakati wa likizo, ili kuwaepusha na wimbi la vitendo vya ukatili wa kijinsia katika ulimwengu wa sasa wa sayansi na teknolojia.

 

Aidha, amepiga marufuku suala la watoto kubebwa kwenye bodaboda, akisema ni hatari kwa usalama wao, na kwamba yeyote atakayebainika kufanya hivyo atachukuliwa hatua kali za kisheria.

 


Katibu tawala huyo amebainisha hayo jana katika sherehe za mahafali ya nne ya Watoto waliohitimu elimu ya awali katika shule ya Kimataifa ya Monti iliyopo Mikocheni jijini Dar es Salaam.

 

“Kama serikali tunawakumbusha wazazi umuhimu wa kuwa karibu na watoto wao kwa sababu ukiangalia dunia inavyokwenda, tunahitaji mawasiliano ya karibu kati ya mzazi na mwalimu anayemwangalia mtoto akiwa shuleni, pamoja na kujua wanachanganyika na watu gani wanaporudi nyumbani,” amesisitiza Warda huku akiipongeza Shule ya Kimataifa ya Monti kwa kuibua na kulea vipaji vya watoto ili kuendana na mabadiliko ya kiteknolojia katika dunia ya sasa.

 

Pia ameeleza kufarijika na malezi pamoja na elimu ya kisasa wanayopatiwa watoto hao na kuahidi kuwa Serikali itaendelea kushirikiana na uongozi wa shule hiyo inayotumia mtaala wa kimataifa wa Cambridge unaozingatia kiwango cha kimataifa cha elimu na kutambuliwa na vyuo vikuu na waajiri kote duniani.

Akizungumzia mahali hayo, Mkurugenzi Mkuu na mmiliki wa shule hiyo, Fatma Fernandes amesema shule hiyo inampokea mtoto mwenye umri kuanzia mwaka mmoja na kuendelea kisha kumlea na kumkuza kielimu hadi anapofikisha umri wa miaka mitano ndipo anapoanza darasa la kwanza.

 


“Kwa elimu ya msingi watoto wanasoma kwa miaka sita. Shule ina matarajio makubwa ikiwemo kujenga miundombinu inayolenga kuunga mkono vipaji vya watoto. Mfano tunajenga ‘swimming pool’ kwa wale wanaopenda kujifunza kuoegelea, pia tutajenga viwanja vya mchezo wa mpira wa kikapu na tenesi, pia tunajenga kampasi Madale ambayo itakuwa ya msingi na sekondari na ni kutwa na bweni,” amesema.

 

Aidha, amesema wamejikita kuhakikisha watoto wanasoma kompyuta kupitia maabara ya kompyuta iliyopo shule hapo.

 

“Kuhusu matumizi ya AI hatujaangalia tu kwa mtoto lakini pia tumeangalia pia kwa mwalimu ili kurahisisha kazi ya ufundishaji. Kwa sasa kuna School AI ambayo tumeweka kwenye mifumo yetu ambayo inamsaidia mwalimu kumrahisishia kutengeneza mpango kazi wa masomo, mwalimu hatumii tena saa 40 kama zamani, kwa muda mfupi anaweza kutengeneza kila kitu anakwenda darasani na kuwafundisha watoto na kumuelewa,” amesema na kuongeza;

 

“Walimu wamejikita kuelewa AI na kuhakikisha watoto wetu wanaitumia kwa usalama. Kompyuta zetu zote zina mifumo ambayo ni salama kwa watoto kutumia”.

 Kwa upande wake mmoja wa wazazi wenye watoto shuleni hapo, Kaley Milao alieleza kuridhishwa na uwezo wa watoto walionesha katika masomo pamoja na kufikiri.

 


“Tunategemea makubwa kwani wanafungua kampasi kule Madale. Utakuwa ni muendelezo mzuri kwa sababu AI au teknolojia haiepukiki, lazime tuende nayo tuone namna gani tunaitumia kutufaidisha sisi,” amesema.

 

Post a Comment

Previous Post Next Post