VYOMBO VYA HABARI VYA SERIKALI VIWEKE USAWA WA KURIPOTI UCHAGUZI MKUU:NDELWA





Vyombo vya habari vya Serikali vimetakiwa  kuhakikisha vinatoa nafasi sawa ya kuripoti habari kwa vyama vya siasa katika kipindi cha uchaguzi Mkuu Oktoba 2025.

Rai hiyo umetolewa leo Mei 02/2025 na Wakili na Mshauri Wakili wa Mahakama kuu, Mh.Lwijiso Ndwela wakati mahojiano Waandishi nguli wa habari  kwenye mjadala ujulikanao kama "Cafe Talk" ulioandaliwa na Clouds Media, kwa kushirikiana na Crown Media pamoja  na Ayo Tv ikiwa ni kuzungumzia kanuni mbalimbali za uchaguzi zinazosimamiwa na Tume huru ya Taifa ya  Uchaguzi (INEC).

Wakili Ndelwa amesema kuwa kanuni za uchaguzi zinaelekeza vyombo vya habari vya imma kama vile TBC, kutoa nafasi sawa ya kuripoti taarifa ya vyama vya siasa ikiwemo kwenye mikutano ya hadhara,mahojiano maalumu pamoja na mambo mengine ili kuweka usawa wa utoaji wa taarifa kwa vyama hivyo.

"Kanuni hizi za uchaguzi zinatoa maelekezo mbalimbali wakati wa kipindi cha  uchaguzi ikiwemo kuvitaka vyombo vya habari kutoa fursa sawa kwa vyama vya siasa kutangaza taarifa zake,nasio kuendelea chama ilichopo madarakani pekee" amesisitiza Wakili Ndelwa.

Nakuongeza kuwa,"Wakati mwingine vyombo vya habari vya Serikali vimekua havitekelezi kanuni hiyo na kuendelea kufanya upendeleo kwa baadhi ya vyama jambo ambalo ni kinyume na kanuni za uchaguz

Post a Comment

Previous Post Next Post