Mhe. Mchengerwa ang'aa, afunga goli mechi ya marais wa CAF na viongozi wa FIFA na wachezaji nguli duniani.




Na John Mapepele, Arusha 

Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Mohamed Mchengerwa ameibuka  miongoni mwa wachezaji waliong'aa katika mechi ya kihistoria baina ya marais wa mashirikisho ya soka wa mataifa ya Afrika na wachezaji nguli duniani leo Agosti 10, 2022 jijini Arusha.

Mechi hiyo imechezwa jioni ya leo katika eneo la Shule ya St. Constantino baada ya kumalizika mkutano mkuu wa Shirikisho la Soka Barani Afrika( CAF) uliofanyika katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano  cha Arusha na kuhudhuriwa na wageni kutoka nchi 58   duniani.

Katika mechi hiyo,  Mhe. Mohamed Mchengerwa aliifungia timu yake goli baada ya kuwachanganya mabeki  wa timu pinzani.


Kabla ya kuanza kwa mechi hiyo Mhe. Mchengerwa alitoa zawadi  za Serikali kwa viongozi mbalimbali wa FIFA na CAF.

Miongoni mwa viongozi hao ni Rais wa FIFA Gianni Infantino, Rais wa CAF   Patrice Motsepe na Katibu Mkuu wa CAF.

Mhe. Mchengerwa amesema  haya ni mafanikio makubwa kwa Tanzania kuandaa mkutano huo ambao umekwenda kuitangaza Tanzania kimataifa.


Amesema dhamira ya Serikali kwa sasa ni kutumia michezo kuitangaza Tanzania kimataifa.


Post a Comment

Previous Post Next Post