Na Yusuph Digossi-Sauti za Mtaa
Yanga tayari imeshaanza maandalizi ya msimu mpya ambapo wameweka kambi katika Viwanja vya Avic Town Kigamboni na leo ni siku ya tatu tangu waanze mazoezi hivyo Mayele atajiunga na wenzake muda mfupi baada ya kumaliza mapumziko ya msimu uliopita.
Ujio wa mshambuliaji huyo fundi wa kucheka na nyavu ni habari njema kwa mashabki wa Yanga mara baada ya kuripotiwa kuwa nyota huyo anaweza kuondoka Jangwani kwenda kutafuta changamoto mpya sehemu nyingine baada ya mafanikio aliyoyapata msimu uliopita.
Tags:
MICHEZO