Na Yussuph Digossi- Sauti za Mtaa Blog
Mchezo wa Ligi kuu Tanzania bara kati ya wenyeji Geita Gold dhidi ya Yanga hadi sasa ni mapumziko huku vinara wa Ligi kuu Tanzania bara Yanga Sc wakitoka kifua mbele kwa uongozi wa goli moja bila majibu katika Uwanja wa CCM Kirumba Mwanza
Bao la mapema kutoka kwa Kinara wa mabao Fiston Mayele ambaye alitumia vizuri makosa ya walinzi wa Geita Gold limewapa uongozi wananchi katika dakika 45 za kipindi cha kwanza
Timu zote zilianza mchezo kwa kasi ya juu na kushambuliana kwa zamu, Geita Gold walitengeza nafasi kadhaa lakini mshambuliaji George Mpole alikosa umakini katika kumalizia
Yanga imewakosa baadhi ya nyota wao muhimu katika kikosi cha kwanza akiwemo Saido Ntibanzokiza , Khalid Aucho, Farid Mussa , Djuma Shaban na Yacouba Sogne ambaye ni majeruhi wa muda mrefu.
Paul Godfrey , Yasin Mustapha , Deus Kaseke na Salum Abubakar ( SureBoy) wameanza kwenye kikosi cha kwanza wakichukua nafasi za wachezaji waliokosekana
Kipindi cha Pili kinafuata , endelea kutembelea sautizamtaatz.blogspot.com kwa habari mbalimbali na matukio